Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limeendelea kutekeleza mkakati wake wa kuboresha mazingira ya kazi kwa kukabidhi magari sita (6) mapya yenye thamani ya Shilingi milioni 903 kwa Meneja wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano, Meneja wa Network Operations and Maintenance pamoja na Meneja wa Network Planning, hatua inayolenga kuongeza ufanisi wa shughuli za kiutendaji na utoaji wa huduma kwa wananchi.
Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limetunukiwa tuzo ya kutambua mchango wake mkubwa katika kufanikisha Kongamano la Kwanza la Mwaka la Ulinzi wa Taarifa Binafsi na Faragha, baada ya kudhamini huduma ya intaneti ya uhakika iliyowezesha shughuli zote za kongamano hilo kufanyika kwa ufanisi.
TTCL tunamshukuru Naibu Gavana wa Benki Kuu kwa kutembelea banda letu na kwa kutambua mchango wa Shirika katika kujenga Tanzania ya kidijitali.
Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) linaendelea kutumia Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026) kutoa huduma na elimu kwa wananchi kuhusu bidhaa na huduma mbalimbali za mawasiliano zinazotolewa na Shirika hilo.
Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limeandika historia mpya baada ya kutunukiwa Tuzo Maalum na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kufuatia mafanikio ya kurejea kwenye faida kwa mara ya kwanza baada ya kipindi kirefu cha changamoto za kifedha.
Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limejipanga kikamilifu kuhakikisha wateja na wananchi wanaotembelea Banda Na. 26 katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026) wanapata huduma bora, elimu kuhusu bidhaa na huduma mbalimbali za kidijitali, pamoja na suluhisho zinazokidhi mahitaji yao.